Biashara ya Ice Cream ni biashara nyingine nzuri zenye faida ukiwa na malengo makini katika sehemu za mijini.Kampuni kubwa kama azam na nyinginezo zilianza kidogo kidogo kwa kuuza ice cream na kukosa ushindani madhubuti kulifanya kujilimbikizia faida kubwa mno na hatimaye kuwa kampuni kubwa mno huku ikingiza bidhaa zingine sokoni zilizoonekana hazina ushindani mkubwa.Je wewe upo sehemu za mjini kama Said Salim Bakhresa alivyokuwa dar es salaam akaanza kuuza ice cream na kutokeza kampuni kubwa la Azam yenye utajiri zaidi ya Tirilion 2.4TSH(mwaka 2015).
Unachotakiwa kufanya ni kujifunza jinsi ya kutengeza ice cream kozi zinatolewa kwa miezi si zaidi ya miezi mitatu kwa kutumia mashine.Kujifunza kuchanganya sukari,  unga wa ice cream ni muhimu sana katika biashara hii.
Hata kama hauna mtaji mkubwa unaweza kusambaza ice cream zako kwa wateja mbalimbali kama mashuleni, vyuoni, maofisini na n.k.
"Hata mkuyu ulikuwa mche"
Kuwa karibu yetu zaidi Like page yetu Facebook