Ntuseni Nesane ni mojawapo kati ya watu waliofanikiwa sana kwa kujiajiri katika kilimo cha nyanya Africa kusini.Kwa sasa ana miaka 71 na amekuwa katika kilimo cha nyanya kwa zaidi ya miaka 40.Bila kuwa na elimu yoyote, mtaji duni wa punda mmoja na jembe la mkono Ntuseni Nesane amefanikiwa sana.
Kwa sasa, mashamba yake yanazalisha 14,400 Tonne za nyanya kwa msimu pia ameajiri wafanyakazi zaidi ya 200.Kila mwaka anatumia 3million Rand(zaidi ya $200,000, zaidi ya 420MilionTsh) kulipa wafanyakazi pekee.
Kutoka hekari 10 mpaka sasa zaidi ya hekari 400 kwa kulima nyanya.Alianza kwa kuuza nyanya katika masoko ya ndani kwa sasa anasafirisha kwenda Mozambique, Zimbabwe na Botswana.
 Je unajua Aliko Dangote tajiri mkubwa Africa amejiingiza kwenye kilimo cha Nyanya.
Kwa kawaida kuna msemo unaosema kama ukitaka kujua fursa zilipo angalia na kufuata mahali ambapo wenye pesa wanawekeza pesa zao.
Aliko Dangote amewekeza zaidi ya dola 20Million katika biashara ya nyanya.Biashara hiyo ya uzalishaji wa nyanya na kuzisaga kuzalisha TOMATO PASTE maeneo ya Kano, kaskazini mwa Nigeria.Dangote anapanga kuzalisha TOMATO PASTE kadiri iwezakanavyo ana nategemea kushindana na soko la China linaloingiza TOMATO PASTE kwa wingi.Licha ya Aliko Dangote kumiliki viwanda vya cement, sukari, chumvi na unga wa nafaka mbalimbali bado anaona fursa kubwa katika kilimo na biashara ya nyanya.
Bofya LIKE kwenye Facebook page yetu ./ Follow Twitter yetu kwa Mawazo zaidi